Utekaji nyara kikundi cha wasichana ulio fanywa na kikundi cha maasi Kaskazini mwa
Nigeria, takriban mwezi mmoja uliopita, umeamusha hisia na utendaji mkali zaidi kwa
jumuiya ya kimataifa dhidi ya kikundi hicho, ambacho tangu kuanza maasi hakuna vurugu
hata moja iliyofanikisha ushindi katika lengo lake, zaidi ya kuteka nyara wasichana
wa shule.
Uchambuzi uliofanywa na Kirk Ross na kunukuliwa na Allafrica ,
19 Mei 2014, unasema, utekaji nyara huo umekuwa ni mwanzo wa uchunguzi zaidi kwa yale
yaliyokuwa yakipuuzwa kwanza, katika nia za kikundi na matukio mengine ndani ya
Nigeria ambayo yanaweza kuchangia, uelewa juu ya kikundi cha Boko Haram, tabia yake
na vyanzo vya msaada kwa kikundi hicho.
Mwandishi anataja lengo kuu la Boko
Haram, bila shaka ni kupinga elimu ya Magharibi , lakini nia kuu iliyofichika ni
kupinga ushawishi wa maisha ya nchi za Magharibi katika eneo la Kaskazini mwa Nigeria.
Ingawa jina la rasmi la kikundi hiki cha upinzani ni Jama'atu Ahlis Sunna Lidda'awati
wal- Jihad, au "kundi la watu wenye nia kueneza mafundisho ya Mtume na Jihad,
kikundi hiki kimetambuliwa kwa jina la' Boko Haram, mara nyingi hutafsiriwa kuwa
na maana ya elimu wa Magharibi ni haramu , na hivyo moja kwa moja inaonyesha chuki
za kiitikadi dhidi ya watu, taasisi na jumuiya zisizokuwa na Kiislamu.
Wanachama
wa kikundi hicho cha Boko Haram, wanaiona elimu ya Magharibi, kama ni udanganyifu
na ulaghai, unaotafuta kuzamisha idadi kubwa ya watu katika nguvu za Ulaya na hivyo
kudhoofisha maadili ya jadi ya Kaskazini.
Jina Boko Haram, hivyo, linakuwa
na maana ya kuwa kinyume na itikadi za Magharibi kwa ujumla. Lakini wasomi katika
eneo hilo la Kaskazini mwa Nigeria , wanauita utendaji wa Boko Haram kuwa ni msimamo
dhidi ya Mungu na upotoshaji wa maadili ya jadi Kiislam Kaskazini mwa Nigeria.
Ni kubadili maana ya haki na mawazo ya Kimungu na kuwa ni utendaji wenye ukatili
wa kinyama. Maandamano ya Waalimu Walimu nchini Nigeria wamefanya
maandamano ya siku moja, kushinikiza serikali kuharakisha juhudi zake za kuwatafuta
wasichana waliotekwa nyara na kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram kwa
zaidi ya mwezi mmoja sasa. Pia maandanamo yalilenga kupinga mashambulizi ya Boko
Haram dhidi ya walimu. Kiongozi mmoja wa walimu hao aliambia BBC kwamba zaidi ya
walimu mia moja sabini wameuawa mwaka huu. Alituhumu maafisa wa serikali kwa kutoongeza
juhudi za kuwalinda walimu na badala yake kujihusisha zaidi na siasa. Wakati huohuo,
Marekani imetuma vikosi vyake nchini Chad , nchi ambayo inapakana na Nigeria kama
sehemu za juhudi zake kusaidia katika kuwatafuta wasichana waliotekwa nyara.