Umoja wa Mataifa wamkumbuka Profesa Maathai Wangai
Jumanne katika ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa , kulifanyika hafla ya kumuenzi
hayati Profesa Wangari Maathai, kama kumbukumbu ya kupita miaka kumi tangu mwanamke
wa kwanza Mwafrika, kupokea tuzo ya heshima ya amani Mwanahabari Grace Kaneiya
ameripoti kwamba, wakati wa hafla hiyo, Naibu mwakilishi wa kudumu wa Kenya kwenye
Umoja wa Mataifa Balozi Koki Muli Grinyo alimtaja Profesa Maathai aligusa maisha
ya watu mbali mbali na hata kubadili maisha yao. Naye Mshauri maalum wa katibu
mkuu kwa ajili ya ajenda ya baada ya Maazimio ya mwaka 2015, Amina J. Mohammed, alimtaja
Profesa Maathai kuwa kielelezo kwa wote waliokutana naye na kwamba sifa zake zitaishi
sio tu nchini mwake Kenya lakini hata nje ya Kenya. Na kwamba wanapojadili ajenda
za baada ya malengo ya milenia ya mwaka 2015, katika muono wa kuwezesha maisha
yenye hadhi kwa wote, wachukue hatua kwa kufuata amfano wa Profesa Maathai , katika
kuwajali watu wote duniani sawia. Hafla hiyo ilijumuisha uzinduzi wa bamba maalum
lililonakshiwa taarifa kuhusu Profesa Maathai na upandaji wa mti mwingine, karibu
na ti aliopandwa na Wangari Mathai katika eneo la Umoja wa Mataifa. Wangari Muta
Maathai alizaliwa Kenya 1 April 1940 na kufariki dunia 25 Septemba 2011 . Alikuwa
Mkenya Mwanasiasa na mpenzi wa mazingira. Alipata elimu yake katika shule ya Mtakatifu
Scholastica Marekani na pia Chuo Kikuu cha Pittsburgh, na Chuo Kikuu cha Nairobi
nchini Kenya. Katika miaka ya 1970, Maathai alianzisha kikundi cha kujali mazingira
kilicho julikana “Green Belt Movement”, kikundi cha kujitegemea katika kujali mazingira,
kisicho kuwa cha kiserikali, na kililenga zaidi katika juhudi za upandaji wa miti,
uhifadhi wa mazingira, na haki za wanawake. Mwaka 1986, alituzwa tuzo ya Haki ya Maisha,
na mwaka 2004, yeye akawa mwanamke wa kwanza Afrika kwa kupokea Tuzo ya Heshima ya
Amani kwa mchango wake katika maendeleo endelevu, demokrasia na amani. Maathai
aliwahi kuwa mbunge na naibu waziri wa Mazingira na Maliasili wakati wa serikali
ya Rais Mwai Kibaki kati ya Januari 2003 na Novemba 2005. Aidha alikuwa Diwani wa
heshima wa Dunia. Mwaka 2011, Maathai alifariki kwa matatizo ya saratani katika
mirija ya uzazi.