2014-05-20 12:08:42

Wakulima wadogowadogo bado ni muhimu katika upatikanaji wa chakula


Zaidi ya watalaam 800 kutoka sehemu mbalimbali za dunia , walikusanyika pamoja mjini Addis Ababa Ethiopia, kujadili changamoto na uwekezaji unaohitajika kufanikisha lengo la kutokomeza utapiamlo na njaa duniani.
Katika mkutano huo ilielezwa kwamba, wakulima wadogowadogo bado ni nguzo ya uzalishaji wa chakula duniani, kwa utambuzi kwamba, zaidi ya watu milioni 500 ni wakulima wa mashamba madogomadogo ya kifamilia, ambayo huzalisha hadi asilimia 80 ya chakula kinacho tumiwa na nchi zenye viwanda vichache.
Dk Kanayo F. Nwaze , Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo ( IFAD)wakati akishiriki katika mkutano huo wa Kimataifa juu ya Sera za Chakula na Tafiti( IFPRI) 2020, alisisitiza kuwekeza katika mifumo jasiri ya wakulima wadogo wadogo, ambayo imekuwa kwa miaka mingi njia kuu upatikanaji wa chakula cha jamii na uwiano endelevu katika maendeleo ya mataifa."

Kwa mujibu wa IFPRI, ajenda baada ya malengo ya 2015, inapaswa kufuta njaa ifikapo mwaka 2025, lakini hii inaweza tu kufanikiwa " kwa kujenga ujasiri wa mazingira , kisiasa na kiuchumi na kuondokana na majanga mbalimbali yanayo tishia usalama wa chakula na maisha .

Mkuu wa IFAD, alionyesha imani yake kwenye umuhimu wa kujenga ujasiri kwa wakulima wadogo wadogo , ambao bahati mbaya, mara kwa mara hupambana na nyakati ngumu. Alisema , wao bila ya chaguzi, huwekeza katika kilimo hata nyakati za migogoro, wakihatarisha msingi wa mali yao, bila ya kuwa na bima,wala kuwa na dhamana katika huduma za fedha na mifumo ya usalama ya kijamii. Matokeo yake ni kuchukua hatua kali kama vile kuondoa watoto kutoka shule, kuuza kila kitu chao, kukusanyika na kuhamia mijini. Hivyo nchi zinapaswa kusaidia wakulima wadogo wadogo katika kukuza umiliki na uhakika wa ustawi endelevu.

Ripoti iliyotolewa katika kikao hicho iliwaangalisha washiriki wa mkutano kwamba, katika kipindi cha miaka mitano peke yake, dunia imeshuhudia tetemeko kubwa la ardhi huko Haiti ; ukame katika Pembe ya Afrika ; tetemeko la ardhi la tsunami ulio sababisha mgogoro wa nyuklia Japan; na kupanda kwa bei za vyakula mwaka 2008 ambako bado kunaathiri bei za vyakula duniani hata leo . Aidha katika kipindi cha miezi sita peke yake iliyopita, Kimbunga Haiyan kilicho tokea Ufilipino, mafuriko makubwa yaliyopiga Uingereza; vita vya wenyewe kwa wenyewe imeendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati , Syria, na Sudan ya Kusini; maporomoko ya ardhi yaliyo vuruga Afghanistan; na ugonjwa mpya iitwayo katika nji aya pumua hewa mwilini uliojitokeza katika Peninsula ya Arabia, ni maafa yasiyoweza kusahaulika. Nayo Ripoti ya hivi karibuni kutoka Jopo la Kimataifa ya Hali ya Hewa Change ( IPCC) pia alithibitisha jukumu binadamu katika kusababisha mabadiliko ya hali ya hewa na imeonya kutokea kwa majanga zaidi.

Na Mkurugenzi Mkuu wa IFPRI, Sheggen Fan, alisema, kuna uwezekano wa majanga mengi kuzuiwa katika uso wa dunia, iwapo binadamu wote watapania kwa nia moja kujenga mafanikio licha ya kukabiliana majanga. Na hilo litategemea jitihada mpya katika kushirikamana na umoja katika ajenda ya ujasiri.

Aidha ameeleza juhudi za Umoja wa Mataifa kusaidia familia kukabiliana na nyakati ngumu kwa njia endelevu, hufanyika pia kupitia Mpango wa Chakula WFP) ambao hufanya kazi kwa mujibu jadi yake ya kutoa msaada wa chakula, kuchangia asilimia 40 ya shughuli zake na mipango inayo andaliwa na kuhamasisha ujasiri. Dk Ertharin Cousin , Mkurugenzi Mtendaji wa EFP, Pa alielezea imani yake kwamba mchakato wa kufikia ujasiri lazima kuanza na dhana ya kuhama katika kufikiri. " Ujasiri inahitaji uelewa wa maisha ya jamii , " alisema.

Na ni muhimu kuwa na mageuzi ya matazamio na mawazo mapana zaidi umiliki wa mali za kudumu zaidi ya umiliki wa nyumba, na kuingia katika ubia wa sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa kila mwanamme na mwanamke anawezeshwa kuchagia kwa kiwango kikubwa uwezo wake katika maamuzi na utendaji. Na kwamba mahitaji ya dunia yanahitaji kupitishwa kwa ujasiri kutoa gawio linganifu, hata kwa jamii tete ambazo leo hii katika uso kimazingira, kiuchumi, na lishe zinaonekana kufilisika. "

Aliongeza kuwa, jumuiya zilizoathirika na ukame, mafuriko , na majanga mengine, mbinu ya ujasiri inaruhusu uchukuaji wa hatua za kina kurudisha maeneo ya kuishi na uzalishaji kwa lengo la kboresha ustawi wao. Ajenda zenye kuimarisha ujasiri zitawezesha familia kuwa imara na kuhimili mshtuko, na hivyo kurudi katika juhudi za uazalishaji hasa chakula kwa ajili yao na watoto wao.









All the contents on this site are copyrighted ©.