2014-05-19 15:02:42

Poland inamkaribisha Papa Francisko kwa mikono miwili mwaka 2016


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 19 Mei 2014 amekutana na kuzungumza na Waziri mkuu wa Poland Bwana Donald Tusk, ambaye baadaye alikutana na kuzungumza pia na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Katika majadiliano ya viongozi hawa wawili wamegusia kwa namna ya pekee tukio la Mama Kanisa kumtangaza Yohane Paulo II kuwa Mtakatifu na umuhimu wake nchini Poland. Waziri mkuu Tusk anamkaribisha kwa mikono miwili Baba Mtakatifu Francisko nchini Poland kunako mwaka 2016 wakati wa maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani. Viongozi hawa pia wameangalia hali ya uchumi na kijamii nchini Poland pamoja na kuchambua hali ilivyo katika Jumuiya ya Kimataifa kwa sasa kwa kuonesha wasi wasi kutokana na kinzani zilizopo Ulaya Mashariki.







All the contents on this site are copyrighted ©.