2014-05-17 10:10:10

Maandalizi ya Sinodi ya Maaskofu yapamba moto!


Sekretarieti ya Sinodi za Maaskofu imehitimisha kikao chake cha siku mbili kilichofanyika kuanzia tarehe 13 hadi tarehe 14 Mei, 2014 ili kupembua muswada wa kwanza wa hati ya kutendea kazi kwa ajili ya maadhimisho ya Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, "Intrumentum Laboris". Kikao cha kwanza kimehudhuriwa na Baba Mtakatifu Francisko.

Kardinali Lorenzo Baldisseri, Katibu mkuu wa Sinodi za Maaskofu amemshukuru Baba Mtakatifu Francisko kwa barua aliyomwandika pamoja na kumteua katibu mkuu msaidizi Monsinyo Fabio Fabene kuwa Askofu, ili kujenga na kuimarisha mshikamano na umoja wa kitume, jambo msingi na muhimu katika maadhimisho ya Sinodi za Maaskofu.

Wajumbe wamepembua kwa kina na mapana hati ya kutendea kazi na kufanya marekebisho msingi kadiri ya hoja zilizotolewa. Kanuni mpya za maadhimisho ya Sinodi zimewasilishwa na zitaanza kutumika hivi karibuni. Mkutano huu wa siku mbili umewahusisha wadau wakuu katika maadhimisho ya Sinodi Maalum ya Maaskofu kwa ajili ya familia, itakayoadhimishwa mjini Vatican, Mwezi Oktoba, 2014.







All the contents on this site are copyrighted ©.