2014-05-16 07:59:13

Gavana mkuu wa New Zealand akutana na Papa mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 15 Mei 2014 amekutana na kuzungumza na Gavana mkuu wa New Zealand Bwana Jerry Mateparae ambaye baadaye amkutana na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Katika mazungumzo yao, viongozi hawa wawili wamejikita zaidi katika maisha ya kijamii na kiuchumi nchini New Zealand sanjari na mchango wa Kanisa Katoliki katika ustawi na maendeleo ya wananchi katika medani mbali mbali za maisha. Wamebadilishana mawazo kuhusiana na masuala ya kimataifa, lakini kwa namna ya pekee mchakato wa ushirikiano wa kikanda katika mikakati ya maendeleo endelevu pamoja na ushiriki wa utunzaji wa amani sehemu mbali mbali za dunia.







All the contents on this site are copyrighted ©.