2014-05-15 11:36:50

Yachachueni malimwengu kwa utakatifu wa maisha!


Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican anawapongeza washiriki wa kongamano la kitaifa nchini Ufilippini, lililojikita katika kuchambua umuhimu wa familia ambao unatoa fursa kwa watu kujifunza kuishi na watu wengine licha ya tofauti zao, kwa kutambua kwamba, wote ni wamoja!

Kongamano hili limezinduliwa hapo tarehe 13 na kufungwa rasmi tarehe 16 Mei 2014, kwa kuwashirikisha viongozi wa Kanisa na waamini walei, ambao Baba Mtakatifu anawataka kuimarisha imani na umoja miongoni mwao chini ya usimamizi wa Khalifa wa Mtakatifu Petro na Maaskofu wao, ili waweze kuwa kweli ni chachu ya kuyatakatifuza malimwengu kwa uwepo endelevu wa upendo wa Kristo kati ya wanadamu.

Baba Mtakatifu Francisko anahitimisha ujumbe wake kwa kuwaweka washiriki wa kongamano hili chini ya ulinzi wa Bikira Maria Mama wa Kanisa na Mtakatifu Yosefu pamoja na kuwapatia baraka zake za kitume!







All the contents on this site are copyrighted ©.