Wasifu wa mabalozi wapya waliowasilisha hati zao za utambulisho mjini Vatican
Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 15 Mei 2014 amepokea hati za utambulisho
kutoka kwa Mabalozi wa Uswiss, Liberia, Ethiopia, Sudan, Jamaica, Afrika ya Kusini
na India.
Balozi Pierre- Yves FUX kutoka Uswiss, alizaliwa kunako tarehe 2
Julai 1976, bado hajaoa. Alipata shahada yake ya uzamili kunako mwaka 1990 na baadaye
mwaka 1994 akafuzu shahada ya uzamivu katika Falsafa. Amewahi kufanya kazi kwenye
balozi za Uswiss nchini Israel, Japan, Iran na baadaye aliteuliwa kuwa Mratibu wa
mgawanyo wa kazi Wizara ya mambo ya nchi za nje. Kuanzia Mwaka 2013 aliteuliwa kuwa
Balozi wa Uswiss Berna ambako anaishi hadi sasa.
Balozi Margaret Ann Louise
JOBSON kutoka Jamaica, alizaliwa kunako tarehe 14 Machi 1955, ameolewa na ana mtoto
mmoja. Alipata shahada yake ya uzamivu kutoka katika Chuo Kikuu cha West Indies kunako
mwaka 1977 na baadaye akajiendeleza katika masuala ya rasilimali watu na kufuzu katika
shahada ya uzamili. Kwa miaka kadhaa alijihusisha na masuala ya tafiti; msimamizi
na mshauri wa masuala ya lugha, mshauri wa UNESCO katika mkoa wa Caraib, baadaye akaajiriwa
na UNDP katika nyadhifa mbali mbali. Kunako mwaka 2003 - 2013 aliteuliwa kuwa Katibu
mkuu msaidizi Wizara ya mambo ya nchi za nje na biashara ya kimataifa. Mwezi Novemba
2013 aliteuliwa kuwa Balozi wa Jamaica nchini Ujerumani ambako anaishi hadi sasa.
Balozi
Rudolf P. Von Ballmoos kutoka Liberia, alizaliwa tarehe 9 Julai 1960 ameoa. Alijipatia
shahada ya uzamivu katika sayansi za kisiasa kunako mwaka 1983 na baadaye akajiendeleza
katika masuala ya maendeleo kimataifa na kujipatia diploma kunako mwaka 1985, huko
Berlin. Amewahi kufanya kazi kwenye Wizara ya Mambo ya nchi za nje Liberia kati ya
mwaka 1979 - 1985; mshauri wa ubalozi nchini Uingereza na Balozi kamili nchini Ghana
kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2013. Mwezi agosti 2013 aliteuliwa kuwa Balozi wa Liberia
nchini Uingereza ambako anaishi hadi sasa.
Balozi Claudina Ntini Ramosepele,
alizaliwa mjini Soweto kunako tarehe 11 Aprili 1957, ameolewa. Kunako mwaka 1988 alijipatia
shahada ya uzamili katika uandishi wa habari kutoka Chuo kikuu cha Patrick Lumumba,
Moscow, Russia. Amewahi kuwa mfanyakazi katika Wizara ya mambo ya nchi za nje ya Afrika
ya Kusini, Katibu wa Ubalozi wa Afrika ya Kusini nchini Canada, Mshauri wa ubalozi
wa Ubalozi wa Afrika ya Kusini, nchini Uingereza, Cameroon na mkurugenzi mkuu wa masuala
haki za binadamu wizarani. Mwaka 2013 akateuliwa kuwa Balozi na sasa anaishi Berna.
Balozi
Nega Tsegaye Tessema kutoka Ethiopia, alizaliwa tarehe 30 Novemba 1966, ameoa na ana
watoto watatu. Ni mtaalam wa uchumi kwa shahada ya uzamivu aliyojipatia kutoka Chuo
kikuu cha Addis Ababa, Ethiopia na baadaye akajipatia shahada ya uzamili katika masuala
ya viwanda huko Uingereza. Kwa miaka mingi alikuwa ni mtaalam wa masuala ya uchumi
Wizara ya madini na nishati; mkurugenzi wa maendeleo ya viwanda, Spika, mshauri wa
masuala ya kijamii katika Ofisi ya waziri mkuu, Waziri wa mambo ya nchi za nje na
mwaka 2013 akateuliwa kuwa ni Balozi wa Ethiopia nchini Ufaransa anakoishi hadi sasa.
Balozi
Mysore Kanpaniah Lokesh, kutoka India, alizaliwa tarehe 20 Mei 1955 ameoa na ana watoto
wawili. Amewahi kuwa mfanyakazi katika Wizara ya mambo ya nchi za nje, katibu Ubalozi
wa India nchini Colombia, Ubelgiji, India, Lagos, Afrika ya Kusini, USA. Kati ya mwaka
2010 hadi mwaka 2013 alikuwa ni Balozi wa India katika Falme za Kiarabu. Tangu Desemba
2013 anaishi Berna.
Balozi Nasreldin Ahmed Wali Abdeltif kutoka Sudan alizaliwa
kumnako tarehe 8 Julai 1960 ameoa na ana watoto watatu. Ni mtaalam wa lugha kwa shahada
ya uzamili aliyojipatia huko Iraq, sheria za kimataifa huko Aia na ana diplomasa ya
uhusiano wa kimataifa aliyojipatia kutoka Ufaransa. Amewahi kufanya kazi Wizarani,
kwenye Ubalozi wa Sudan huko Morocco, Chad, Umoja wa Mataifa, USA na mkurugenzi wa
masuala ya uhusiano wa kimataifa na Marekani. Kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2013 alikuwa
ni Balozi nchini Rwanda. Mwaka 2013 akateuliwa kuwa Balozi wa Sudan, nchini Ufaransa
anakoishi kadi sasa.