Shukrani na pongezi kwa Jeshi la Polisi Italia kwa kuadhimisha Miaka 162 tangu akuanzishwa!
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro
Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Italia, Kamanda
Alesandro Pinsa anapenda kulishukuru kwa dhati Jeshi la Polisi Italia kwa huduma ya
ulinzi na usalama linalotoa kwa wananchi, kwa takribani miaka 162 tangu lilipoanzishwa.
Baba Mtakatifu anatambua fika mchango unaotolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana
na Mji wa Vatican katika kusimamia matukio mbali mbali yanayohusu maisha na utume
wa Kanisa.