2014-05-08 15:19:30

Vatican na Uturuki kuendeleza majadiliano ya kidini


Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini, Alhamisi tarehe 8 Mei 2014 limefanya mkutano na ujumbe wa Rais kutoka Uturuki unaoshughulikia masuala ya kidini (Dyanet), ili kuangalia uwezekano wa pande hizi mbili kushirikiana kwa karibu zaidi, kama ilivyokuwa imependekezwa kunako mwaka 2002.

Mwezi Septemba, 2012, viongozi wakuu wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya kidini walikutana na ujumbe kutoka Uturuki, ili kuangalia na kuweka mikakati ya utekelezaji wa maazimio yaliyokuwa yamefikiwa katika hatua za awali. Mwezi Mei, 2013, ujumbe kutoka Baraza la Kipapa la Majadiliano ya kidini, ulitembelea Uturuki ili kufafanua mambo msingi ambayo pande hizi mbili zingependa kushirikiana. Mkutano uliofanyika mjini Vatican, imekuwa ni fursa ya kutathmini uhusiano wa pande hizi mbili katika mchakato wa majadiliano ya kidini.







All the contents on this site are copyrighted ©.