Mshikamano wa Papa na wananchi wa Afghanstan na Ukraine
Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Sala ya Malkia wa mbingu, Jumapili iliyopita,
tarehe 4 Mei 2014 kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, amewaalika
waamini na watu wote wenye mapenzi mema kuungana pamoja naye katika sala kwa Bikira
Maria kwa ajili ya wananchi wa Ukraine ili vita na kinzani za kijamii ziweze kukoma
na watu waanze kujikita katika amani na udugu.
Baba Mtakatifu Francisko amewakumbuka
na kuwaombea watu ambao wamefariki dunia hivi karibuni kwa kufukiwa na maporomoko
ya udongo huko Afghanistan, ili waweze kuonja huruma ya Mungu na kuwapokea katika
amani ya milele. Anapenda kuwatia shime wote waliosalimika katika janga hili kusonga
mbele kwa njia ya msaada wa wasamaria wema wanaojitahidi kuwapunguzia mateso na mahangaiko!
Mwishoni,
Baba Mtakatifu ameungana na Baraza la Maaskofu Katoliki Italia katika maadhimisho
ya siku ya tisini ya Chuo Kikuu cha Moyo Mtakatifu wa Yesu yanayoongozwa na kauli
mbiu "pamoja na vijana wahusika wakuu kwa siku za usoni". Baba Mtakatifu anasema,
anaendelea kukiombea Chuo Kikuu cha Moyo Mtakatifu wa Yesu ili kidumu katika uaminifu
na utume wake. Panapo majaliwa katika maadhimisho ya Jubilee ya Miaka 50 atatembelea
Kitivo cha tiba na upasuaji pamoja na Hospitali ya Gemelli, iliyoko mjini Roma.
Baba
Mtakatifu amewashukuru na kuwapongeza wanachama wa "Meter" ambao kwa muda wa miaka
ishirini wamekuwa mstari wa mbele katika kulinda na kutetea haki msingi za watoto.
Amewapongeza pia waamini na watu wote wenye mapenzi mema walioungana katika maandamano
ya kutetea zawadi ya maisha!