Askofu Gervas Nyaisonga asimikwa rasmi Jimbo Katoliki Mpanda
Askofu mkuu Francisco Montecillo Padilla, Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Jumapili
tarehe 4 Mei 2014 ameadhimisha Ibada ya kumsimika rasmi Askofu Gervas Nyaisonga kuwa
Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Mpanda. Ibada hii imehudhuriwa na Maaskofu na viongozi
mbali mbali kutoka ndani na nje ya Jimbo Katoliki Mpanda.
Katika mapokezi
ya Askofu Nyaisonga Jimboni Mpanda, Padre Martini Kapufi (42) aliyekuwa Paroko wa
Parokia ya Mwese, Jimbo katoliki Mpanda na Katekista Patrick Mwendowasaa (60) walifariki
dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka baada ya kuacha njia. Waliolazwa
hospitalini kwa matibabu zaidi ni Katekista Daud Saveli na Melkior Malaluma, mwamini.