Askofu mkuu Martin Kreb ateuliwa kuwa Balozi Mpya wa Vatican Visiwani Marshall na
Nauru
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu mkuu Martin Krebs kuwa Balozi mpya wa Vatican
kwenye Visiwa vya Marshall na Nauru. Ataendelea pia kuwa ni Balozi wa Vatican huko
New Zealand Visiwa vya Cook, Fiji, Kribati, Palau, Samoa, Shirikisho la Micronesia,
Tonga, Vanuatu na mwakilishi wa kitume kwenye Bahari ya Pacific.