2014-05-02 08:03:36

Kumekucha Jimbo Katoliki Monze, Zambia!


Askofu mteule Moses Hamungole wa Jimbo Katoliki Monze, Zambia aliyeteuliwa hivi karibuni na Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa kuwekwa wakfu na hatimaye kusimikwa kuwa Askofu Monze, Jumamosi tarehe 3 Mei 2014. RealAudioMP3

Padre Chrisantus Ndaga, Katibu wa Idara ya habari, Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na Kati, AMECEA anasema kwamba, Askofu mteule Moses ni fahari ya Idara ya habari ya AMECEA kwani anakuwa ni Askofu wa tatu katika orodha ya Maaskofu waliowahi kuteuliwa kutoka Idara hii. Wa kwanza alikuwa ni Askofu Joseph Mkwaya na Askofu Fortunatus Lukanima; Maaskofu wote wawili wamekwisha kufariki dunia.

Padre Ndaga anasema, katika Ibada ya Misa Takatifu ya kuwekwa wakfu na hatimaye kusimikwa, ujumbe wa AMECEA unapenda kushiriki kikamilifu kwa njia ya uwepo na mshikamano wa sala, wakati huu Askofu Mteule Moses Hamungole anapopewa utume wa kuongoza, kufundisha na kuwatakatifuza watu wa Mungu Jimbo Katoliki la Monze, Zambia. AMECEA itaendelea kushirikiana na na Jimbo Katoliki Monze kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Monze na AMECEA katika ujumla wake.







All the contents on this site are copyrighted ©.