Chama cha upinzani nchini Zimbabwe MDC kimepata mpasuko mkubwa baada ya aliyekuwa
Waziri mkuu wa Zimbabwe Bwana Morgan Tsvangirai kuondolewa kwenye Chama kwa shutuma
za kutaka kuwadhibiti wapinzani wake ndani ya chama kinyume cha kanuni na taratibu
za kidemokrasia.
Kundi la upinzani linaundwa na Bwana Tendai Biti, aliyekuwa
Waziri wa fedha katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa nchini Zimbabwe. Wachunguzi wa
mambo ya kisiasa wanasema kwamba, Bwana Tsvangiraia akitaka kumdhibiti na hatimaye
kummaliza kisiasa Bwana Tendai Biti.
Mpasuko huu mkubwa ambao hujawahi kutokea
umeendelea kukidhohofisha chama cha MDC ambacho katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka
uliopita kilishindwa kufua damu mbele ya Rais Robert Mugabe aliyeibuka kidedea!