2014-04-27 11:09:26

Watu wamekesha kwa sala, katekesi na tafakari


Waamini waliokuwa wamefurika mjini Vatican kwa ajili ya kushiriki Ibada ya Misa Takatifu ya kuwatangaza Wenyeheri Yohane XXIII na Yohane Paulo II kuwa watakatifu, walifanya kesha la sala na tafakari ya Neno la Mungu pamoja na mafundisho ya Wenyeheri Yohane XXIII na Yohane Paulo II kwatika Makanisa mbali mbali Jimbo kuu la Roma. Ulikuwa ni usiku wa mshikamano katika maisha ya kiroho, kwa kufanya toba na maungano ya dhambi, tayari kushiriki katika Ibada ya Misa takatifu, Jumapili tarehe 27 Aprili 2014.

Pamoja na hali mbaya ya hewa iliyojitokeza Jumamosi, Jioni, lakini bado makundi makubwa ya waamini waliokuwa wakipeperusha bendera na kuimba nyimbo, yalionekana yakitembea kwenye mitaa na viunga vya mji wa Roma bila wasi wasi, ili kushiriki: Ibada na Katekesi mbali mbali zilizokuwa zinatolewa kwenye Makanisa. Baadhi ya waamini walilala karibu na viunga vya Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, ili kuhakikisha kwamba, wanashiriki kwa ukaribu zaidi katika tukio hili la kihistoria, ambalo Mwenyezi Mungu ameliwezesha Kanisa katika mapambazuko ya Millenia ya tatu ya Ukristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.