2014-04-27 10:39:09

Ujumbe kutoka Afrika uliofika mjini Vatican


Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kuwatangaza Wenyeheri Yohane XXIII na Yohane Paulo II kuwa watakatifu imehudhuriwa na umati mkubwa wa waamini na watu wenye mapenzi mema kutoka sehemu mbali mbali za duni.

Marais kutoka Barani Afrika waliohudhuria katika Ibada hii ni: Rais Paulo Biya kutoka Cameroon, Rais Ali Bongo Ondinba kutoka Gabon na Rais Robert Mugabe kutoka Zimbabwe.

Taarifa rasmi inaonesha kwamba, kulikuwa na ujumbe wa waamini kutoka katika dini mbali mbali. Kutoka Afrika kulikuwa na ujumbe wa: Serikali ya Angola, Burkina Faso, Burundi, Cameroon Cape Verde, Pwani ya Pembe, Gabon, Ghana, Guinea Bissau, Equitorial Guinea, Lesotho, Liberia, Msumbiji, Namibia, Niger, Nigeria, DRC, Sudan, Tanzania, Togo, Uganda, na Zimbabwe.







All the contents on this site are copyrighted ©.