2014-04-25 15:53:03

Ushuhuda wa utakatifu wa maisha, kadiri ya wale walioishi nao karibu!


Monsinyo Battista Angelo Pansa ni kati ya wataalam wa maandishi na historia ya Baba Mtakatifu Yohane XXIII, ambaye ameonesha jinsi ambavyo Papa Yohane XXIII tangu akiwa kijana alitamani sana maisha ya Upadre, kwa ajili ya kuwasaidia maskini katika maisha yao ya kiroho.

Ni Papa aliyeanza kuonesha cheche za mageuzi katika maisha na utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro. Akatembelea Hospitali na Magereza ya Roma ili kukutana na kuzungumza na wagonjwa pamoja na wafungwa. Aliithubutu kuanzisha maadhimisho ya Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican, akasafiri kwa Treni hadi Assisi na Loreto kunako Mwaka 1962.

Alikuwa ni kiongozi aliyesimama kidete kulinda na kutetea misingi ya haki, amani, utulivu na maendeleo ya wengi. Alikuwa na Ibada kwa Bikira Maria aliyemsindikiza daima katika maisha na utume wake. Kwa wasaidizi wake wa karibu aliwataka kupiga magoti mbele ya Sakramenti kuu na wala si kwake!

Monsinyo Marco Frisina ambaye kwa miaka thelathini amekuwa ni kiongozi mkuu wa kwaya ya Jimbo kuu la Roma anasema, maisha ya Mwenyeheri Yohane Paulo II yamejikita katika imani na sanaa ni kiongozi aliyependa muziki na kwamba, kwa njia ya muziki, ujumbe wa Neno la Mungu ulikuwa unawafikia wengi.







All the contents on this site are copyrighted ©.