Tunataka Katiba itakayodumisha misingi ya haki, amani na mshikamano wa kitaifa!
Mama Helan Moshi kutoka Jimbo kuu la Dar es Salaam ni kati ya mahujaji kutoka sehemu
mbali mbali waliofika mjini Roma ili kushuhudia Wenyeheri Yohane XXIII na Yohane Paulo
II walitangazwa kuwa Watakatifu, Jumapili ijayo kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu
Petro mjini Vatican.
Anasema, wakati
huu anapofanya hija ya maisha ya kiroho ili kumshukuru Mungu kwa kuliwezesha Kanisa
kupata miamba haw wa imani, sala na mawazo yake bado anayaelekeza Tanzania, akiwaomba
Wenyeheri hawa kuiombea Tanzania ili iweze kuwa na amani, upendo na mshikamano wa
kitaifa.
Anawasihi sana wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutambua kwamba,
wameteuliwa ili kuwawakilisha watanzania wenzao katika mchakato nyeti wa kutunga Katiba
Mpya ambyo ni sheria mama. Hii ni dhamana nyeti, inayopaswa kutekelezwa kwa uadilifu
na weledi mkubwa; hekima na unyofu, ili kweli amani, upendo na mshikamano miongoni
mwa watanzania uendelee kudumu!