Kuweni macho na watu wanaodai kupigiwa simu na Papa Francisko!
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anafafanua kwamba, katika maisha
na utume wake, Baba Mtakatifu Francisko amekuwa akizungumza na watu mbali mbali kwa
njia ya simu, kama sehemu ya mkakati wake wa shughuli za kichungaji.
Huu si
utume wa Baba Mtakatifu katika maisha ya hadhara, kumbe, Idara ya habari mjini Vatican
haina sababu na wala hakuna sababu ya kusubiri maelezo na ufafanuzi wa kina kutoka
Vatican kuhusiana na mazungumzo ya simu yanayofanywa na Baba Mtakatifu Francisko.
Padre
Lombardi anasema, baadhi ya taarifa zilizosambazwa na baadhi ya vyombo vya habari
kinyume kabisa cha matakwa ya mawasiliano kati ya Baba Mtakatifu Francisko na wahusika
hazina ukweli wowote, ni habari za kuzusha zinazotaka kuwachanganya watu. Waamini
na watu wote wenye mapenzi mema, wanapaswa kuwa makini kuhusiana na habari hizi mintarafu
Mafundisho Tanzu ya Kanisa.