Vijana 8,000 kutoka Jimbo kuu la Milano, Kaskazini mwa Italia, Jumatano, tarehe 23
Aprili 2014 wanatarajiwa kushiriki katika Katekesi ya Baba Mtakatifu Francisko na
baadaye kuungama imani yao katika Makaburi ya miamba wa imani, ni watu waliyothubutu
kuyamimina maisha yao kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake.
Hawa ni Mtakatifu
Petro na Paulo. Lengo la hija hii ya maisha ya kiroho ni kuamsha ari na mwamko wa
imani miongoni mwa vijana, ili waweze kuwa kweli ni mashahidi wa Kristo Mfufuka katika
maisha yao!
Kardinali Angelo Comastri, Mhudumu mkuu wa Kanisa kuu la Mtakatifu
Petro mjini Vatican, ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa vijana hawa kwenye Kanisa
kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, siku ya Jumanne, tarehe 22 Aprili 2014. Ibada
hii imewashirikisha Mapadre mia mbili pamoja na umati mkubwa kwa walezi, wanaowasindikiza
vijana hawa katika hija ya maisha yao ya kiroho.
Vijana wanafundwa namna ya
kuheshimiana pamoja na kufanya maamuzi muhimu katika maisha yao, huku wakiendelea
na malezi Parokiani mwao, ili kujenga na kuliimarisha Kanisa. Hija hii pia ni sehemu
ya kumbu kumbu ya miaka mia moja tangu Jimbo Katoliki la Milano lilipoanzisha vituo
vya kulelea vijana Parokiani.