Alhamisi Kuu Papa Francisko alihimiza kutumikiana kwa upendo
Katika ishara ya unyenyekevu na huduma, na kwa mwanga wa kumwiga Kristo , Papa Francisko,
alivaa dramatic, alama ya huduma na kupiga magoti na kuwaosha miguu wagonjwa 12 katika
kituo cha huduma kwa Wagonjwa walemavu cha mjini Roma , wakati akiongoza Ibada ya
Alhamisi kuu jioni “ Coena Domini”. Mapema Alhamisi Papa aliongoza Ibada ya kubariki
mafuta ya Mpako wa wokovu “Krisma”, ambayo pia ni ilikuwa ni Siku Kuu ya Mapadre wote.
Katika Ibada hii Papa aliwakumbusha Mapadre wote kwamba , kukubali kupakwa mafuta
ya kuwa kuhani ni kukubali kuwa mtumishi wa wote na ni zawadi ya utumishi ya kudumu
milele. Hivyo Furaha ya upadre haina mwisho , ni zawadi ya uadilifu, uaminifu na utii
kwa Bwana. Na wakati wa Ibada ya Karamu ya mwisho, Papa licha ya kuonekana mchovu,
na kusaidiwa kupiga magoti na kusimama, aliongoza liturujia ya kuosha miguu ya wagonjwa
12 waliokuwa wameandaliwa, katika kituo cha kuhudumia wagojwa cha St Maria della Provvidenza
Foundation Roma . Kwa huruma na upendo mkuu, Papa alimwendea kila mmoja wao na kumwosha
mguu , kuikausha na kisha kuubusu, kama ishara ya sadaka ya upendo na kumtazama
usoni kwa makini, kulingana na hali ya afya ya mgonjwa . Wagonjwa hao walikuwa na
umri kati ya miaka 16-86 , na wote wanakabiliwa na ulemavu mbalimbali. Wengi walikuwa
ni raia wa Italia, watatu wakiwa na asili ya makabila ya mbali mmoja wao akiwa ni
Muislim.
Kituo hiki cha Santa Maria della Provvidenza, ni kati ya vituo 12
vya huduma ya afya vinavyoendeshwa Shirika la Don Carlo Gnocchi Foundation. Ibada
hii iliweza kutoa tafakari makini katika tabia ya kituo hicho cha afya na kwa Wakristo,
wanao fanya kazi ya kujitolea katika kituo hiki cha wagonjwa walemavu, hasa kwa siku
za Jumapili ambamo huchanganyika na wagonjwa katika kuadhmisha Ibada ya Misa na kumtukuza
Mungu kwa nyimbo . Wengi wa wagonjwa wa kituo hiki ni wagonjwa wasioweza kutembea
na hivyo wengi wao hutumia baiskeli za wagonjwa.
Ibada hii ya kukumbuka Karamu
ya mwisho ya Bwana na mitume wake , na liturujia kuosha yake ya miguu yao, kama
ishara ya huduma, na uzinduzi wa Sakramenti ya Ekaristi , huashiria mwanzo wa kipindi
cha Siku Tatu Kuu za Pasaka “ Triduum”.
Uchaguzi wa Papa wa kuadhimisha mwanzo
wa Siku Tatu Kuu za Pasaka kwa ishara yake ya kuosha miguu ya watu 12 wenye ulemavu
ilikuwa na lengo la kusisitiza aina ya udhaifu, ambayo jumuiya ya Kikristo inaitwa
kutambua mateso ya Kristo, ambayo ni lazima kujishughulisha nayo kwa makini , mshikamano
na upendo .
Katika hotuba yake fupi , Papa alikumbusha kwamba Mungu alijifanya
mtumishi kupitia mwanae Kristo na huu ni urithi wa waamini wote. Kristo alikuja upendo
na wafuasi wake wanapasa pia kutoa jibu la upendo la kuwa watumishi katika upendo.
Na alizamisha zaidi upendo huo akisema, kuosha miguu ya mwingine, wakati wa Yesu
, ilikuwa ni kazi ya mtumwa au mtumishi wa nyumbani. Katika utekelezaji wa ishara
hii , Yesu anawaambia wafuasi wake kwamba wao wameitwa kuwa watumishi kwa kila mmoja,
hata mtu mdogo sana asiyeonekana kuwa na maana katika jamii.
"Kila mtu hapa
lazima kufikiria wengine ... na jinsi ya kuwatumikia wengine kuwa ubora zaidi," alisema
.
Huu ni mwaka wa pili Papa kuadhimisha Misa ya Bwana Karamu ya Mwisho kati
ya kundi la watu wa kawaida walio tengwa na jamii. Mwaka jana, Papa sherehe Misa
ya Bwana Karamu ya Mwisho katika kituo cha Gereza la vijana na watoto watukutu