Papa mstaafu Benedikto XVI asherehekea miaka 87 ya kuzaliwa kwake!
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI, Jumatano tarehe 16 Aprili 2014 ameadhimisha
Miaka 87 tangu alipozaliwa, kwa kusali, kutafakari na kumshukuru Mungu kwa matendo
makuu aliyoweza kumkirimia katika maisha yake hadi wakati huu. Kutokana na Siku hii
kuangukia kwenye Juma takatifu, Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita anasema
Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican kwamba, ameamua kuiadhimisha katika
hali ya utulivu na ukimya pasi na makuu.
Wakati huo huo, Baba Mtakatifu Francisko,
Siku ya Jumatano amempigia simu na kuzungumza na Papa mstaafu Benedikto wa kumi na
sita, kwa kumtakia heri na baraka anapoadhimisha Siku kuu yake ya kuzaliwa. Anasema
amemkumbuka katika sala na sadaka ya Misa Takatifu, Jumatano, kwenye Kikanisa cha
Mtakatifu Martha, kilichoko mjini Vatican.