Majina kadhaa yaidhinishwa na Papa katika mchakato wa utakatifu
Jumanne, Aprili 15, 2014 , Baba Mtakatifu Francisko , alikutana katika hali ya faragha
na Kardinali Angelo Amato, Mkuu wa Shirika kwa ajili ya utajaji wenye Heri na Watakatifu.
Katika majadiliano yao, Papa alikubali miujiza iliyofanywa na watumishi wa Mungu
kadhaa na kuliruhusu Shirika liendelee na Mchakato wa watumishi hao, kutajwa watakatifu.Miujiza
iliyokubali na Papa ni: Muujiza unaohusishwa maombezi ya Mwenyeheri Ludovico ya
Casoria , Padre wa Shirika la Ndugu Wadogo na Mwanzilishi wa Usharika wa Masista
wa Mtakatifu Francis wa Elisabettine. Alizaliwa Italia, Machi 11, 1814 na kufariki
Naples (Italia) Machi 30, 1885. Pia muujiza wa maombezi ya Mwenye Heri Amato Ronconi
, wa Kanuni ya Tatu katika Shirika la la Mtakatifu Francisko ,Mwanzilishi wa Makazi
ya mahujaji watu Maskini katika mji wa Saludecio, ambayo sasa ni jengo la mapumziko
ya Mwenye Heri Amato Ronconi ; aliye zaliwa Saludecio (Italia) mwaka 1226 na kufariki
Rimini (Italia) 1292. Pia Papa ametambua fadhila ya kishujaa wa Mtumishi wa Mungu
Maria Alano de Guynot Boismenu , wa Usharika wa Wamisionari wa Moyo Mtakatifu wa Yesu,
aliyekuwa Askofu Mkuu wa jina wa Claudiopolis , na Mwakilishi Kitume wa Papa wa
Papua ; alizaliwa katika Saint- Malo (France) Desemba 27, 1870 na kufariki Kubuna
( Jamhuri ya Visiwa vya Fiji, Oceania) Novemba 5, 1953 ; Na fadhila kishujaa wa
Mtumishi wa Mungu William Janauschek , Padre wa Shirika la Mapadre wa Patakatifu pa
Mkombozi; alizaliwa mjini Vienna (Austria) 19 Oktoba 1859 na kufariki Juni 30, 1926
.