Baba Mtakatifu Francisko, Jumanne asubuhi tarehe 15 Aprili 2014 amekutana na kuzungumza
na Askofu mstaafu Chabrel Georges Merhi wa Jimbo Katoliki la San Charble en Buenos
Aires, Argentina pamoja na Askofu Marcello Semeraro, Katibu mkuu wa Sekretarieti ya
Makardinali, kwa pamoja wametembelea ofisi mbali mbali za Sekretarieti ya Vatican
ili kusalimiana na viongozi pamoja na wafanyakazi wa Vatican ili kuwapatia kheri na
baraka kwa Siku kuu ya Pasaka ya Bwana.
Wafanyakazi wengi walishangazwa kukutana
uso kwa uso na Baba Mtakatifu wakati wakiendelea na shughuli zao. Huu ni mwelekeo
mpya wa mawasiliano si tu kwa kukutana na makundi makubwa ya watu, bali kila mtu anayo
nafasi katika maisha na utume wa Baba Mtakatifu Francisko. Wafanyakazi wamefurahi,
kwani si rahisi baadhi yao kukutana na Baba Mtakatifu mara kwa mara kutokana na aina
ya kazi walizo nazo!