Rambi rambi za Papa kwa janga la moto Valparaiso Chile.
Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican amepeleka salaam za rambirambi za Papa
Francisko, kwa njia ya telegram kwa Askofu Gonzalo Duarte Garcia De Cortàzar wa Jimbo
la Valparaíso, kufuatia tukio la kusikitisha na moto mkubwa kukuba mji wa Valparaiso.
Papa Francisko, mara baada ya kusikia habari ya kusikitisha ya moto wa kutisha
kutokea katika mji wa Valparaíso, ameonyesha ukaribu wake wa kiroho kwa wakazi wa
mji huo, kwa matoleo ya sadaka ya sala kwa wote walio athirika katika janga hili
na kubwa, akishirikishana uchungu na majonzi ya wale ambao wamepoteza jamaa, makazi
na mali zao. Pia Papa anawakumbuka katika sala zake, kikosi cha uokoaji , pamoja
na mamlaka ya utawala wa jiji na watoaji wa huduma zote za msaada wa kibinadamu, unaotolewa
katika hali ya udugu na mshikamano kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wasipoteze
moyo wa matumaini katika uso wa mashaka.
Pia Papa amepeleka salaam za rambirambi
kwa wafiwa wote. Kwa hisia hizo , Papa anawapa baraka zake maalum za kitume kama
ishara ya upendo kwa Wachile wote.