2014-04-12 08:28:06

Ujumbe wa Pasaka kwa Jumuiya ya Wayahudi Roma


Baba Mtakatifu Francisko amemwandikia ujumbe wa matashi mema na kheri Rabbi mkuu wa Jumuiya ya Wayahudi mjini Roma Bwana Riccardo di Segni kwa ajili ya maadhimisho ya Siku kuu ya Pasaka ya Wayahudi, hapo tarehe 14 Aprili 2014, itakayodumu kwa kipindi cha siku nane.

Jumuiya ya Wayahudi inasema, imepokea kwa furaha na mikono miwili ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko na kwamba, wao pia wanajiandaa kwa ajili ya kumtumia matashi mema katika kipindi cha Pasaka.

Baba Mtakatifu anaiombea amani Jumuiya ya Wayahudi iliyoko mjini Roma, wakati huu wanaposherehekea ushindi wa kukombolewa kutoka utumwamini na mkono wenye nguvu. Pasaka kiwe ni kipindi cha kukuza na kumwilisha huruma, upatanisho na mshikamano wa udugu kwa wote wanaoendelea kuteseka katika utumwa mamboleo.

Baba Mtakatifu anayaelekeza pia mawazo yake mjini Yerusalemu, anakotarajia kutembelea mwezi ujao, anawaomba wamsindikize katika hija hii ya kichungaji kwa njia ya sala zao na kwamba, anaendelea kuwakumbuka na anawatakia baraka tele!







All the contents on this site are copyrighted ©.