Jumapili ya Matawi mjini Roma kuongozwa na Papa Francisko!
Baba Mtakatifu Francisko anatarajiwa, Jumapili ya Matawi, Mama Kanisa anapomsindikiza
Yesu kwa shangwe kuingia mjini Yerusalemu, ili kukabiliana na mateso, kifo na ufufuko
wake, anatarajiwa kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la
Mtakatifu Petro mjini Vatican.
Hii pia ni Siku ya ishirini na tisa ya Vijana
Kijimbo, inayoongozwa na kauli mbiu "Heri maskini wa roho maana ufalme wa mbinguni
ni wao". Baba Mtakatifu atabariki matawi na baadaye maandamano ya vijana yataanza
kuzunguka Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro na mwishoni, Baba Mtakatifu Francisko
ataongoza Ibada ya Misa Takatifu, mwanzo wa Juma kuu.
Hii ni siku ambamo Mama
Kanisa pia anakumbuka miaka thelathini tangu Mwenyeheri Yohane Paulo II alipowakabidhi
vijana Msalaba wa Mwaka wa Ukombozi, Msalaba ambao umetembezwa sehemu mbali mbali
za dunia, kielelezo cha imani, matumaini, mapendo na changamoto kwa vijana wa kizazi
kipya!.