WHO, yatoa mwongozo mpya kwa maradhi ya ini (Hepatitis C)
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani (WHO), limetoa mwongozo mpya kwa ajili
ya matibabu ya maradhi ya ini yanayojulikana kwa jina la “hepatitis C”, maambukizi
sugu yanayotajwa kuathiri kati ya watu 130- 150 milioni duniani.
Mwongozo
mpya una lengo kusaidia nchi kuboresha matibabu na huduma kwa maradhi ya ini na hivyo
kupunguza vifo vinavyotokana na kansa ya ini. Dk Stefan Wiktor ,Mkuu wa Mpango wa
kukabiliana na Maradhi ya ini wa WHO, ameeleza katika ripoti yake.
Mwongozo
huo uliochapishwa , unakwenda sanjari na upatikanaji wa dawa zinazofaa zaidi , kutibu
Hepatitis C, pamoja na ahadi ya dawa mpya zaidi zitakazo tolewa katika miaka michache
ijayo , kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa, unao sababisha vifo 350,000 hadi 500,000
kwa mwaka .
WHO sasa inafanya kazi ya kuingiza mwongozo huo, kama sehemu ya
mipango matibabu ya kitaifa. Msaada wa WHO, ni pamoja na uwezeshaji wa matibabu
mapya, na wazo la uwezekano wa tiba hiyo kupatikana kwa gharama nafuu kwa watu
wote , kama vile uwepo wa vipimo bora kutahimini hali ya ugonjwa na aina ya dawa
inayoitikia vyema kutibu hepatitis C.
Mpaka sasa tiba ya Hepatitis C ni ghali
kwa wagonjwa wengi. Na hivyo, changamoto mpya sasa ni kuhakikisha kwamba kila mtu
anaye hitaji madawa haya, anaweza kuyapata, anasema Dk Peter Beyer , Mshauri kwa ajili
ya Madawa muhimu na vifaa, wa Idara ya Afya , WHO.
Mwongozo mpya , ulizinduliwa
katika mkutano wa Kufungua mwaka 2014 wa Kongamano la Kimataifa, kwa ajili ya maradhi
ya ini , lililofanyika London, ambalo lilikamilika kwa kutoa mapendekezo muhimu tisa
. Mapendekezo hayo ni pamoja na mbinu ya kuongeza idadi ya watu kupimwa maambukizi
ya hepatitis C , ushauri na jinsi ya kukabiliana na uharibifu wa ini kwa wale walioambukizwa
na jinsi ya kuchagua na kutoa matibabu sahihi kwa muda mrefu kwa walioshikwa na hepatitis
C. Hepatitis C huenea kwa njia ya kuwasiliana na damu yenye vimelea, kwa kutumia
pamoja sindano zenye vimelea, kuongezewa damu yenye vimelea, maambukizi kutoka kwa
mama kwa mtoto mchanga wakati wa kujifungua, kwa njia ya kujamiiana, utumiaji wa
sindano chafu kutoa damu kwa ajili ya vipimo, kushirikiana nyembe za kunyolea ndevu,
miswaki, na mambo mengine yanayoweza kuingiza damu yenye vimelea hepatitis C kwa
mtu mwingine.
WHO inasema, mtu hawezi kupata ambukizo la hepatitis C kwa kuishi
au kuwa karibu , au kumgusa mtu mwenye ugonjwa huo, isipokuwa kwa njia zilizotajwa
hapo juu. Aidha kwamba, kwa asilimia 30% chanzo cha maambukizi ya ugonjwa huu hakijulikani
hasa hepatitis C sugu.
Dalili za kuwa na ugonjwa, watalaam wanasema, hakuna
dalili za papo kwa papo wakati wa kwanza wa maambukizi. Takriban ya 80% ya wagonjwa
wapya dalili hazionyeshi nje. Na asilimia 20% iliyobaki ya wagonjwa wapya walioambukizwa
huwa na za uchovu wa mwili, maumivu ya tumbo, kichefuchefu, upungufu wa hamu ya
chakula, au kuwa na dalili za homa ya manjano, ambayo sehemu nyeupe za mwili kama
macho na viganja kuwa na rangi ya njano. Na Wakati huo huo, mkojo inaweza kuwa na
rangi ya hudhurungi. Dalili hizi kwa kawaida hujitokeza baada ya kupita kipindi cha
wiki 4-12 tangu kuambukizwa na HCV. Baadhi ya watu huwa na dalili za joto la mwili
kupanda au homa na wengine hujisikia kama vile wana mafua. Watalaam wanashauri
watu kujenga tabia ya kupima afya mara kwa mara, ili kugundua kasoro mapema katika
maungo ya mwili.