2014-04-07 10:31:45

Mwachieni nafasi Kristo ili afungue makaburi ya mioyo yenu!


Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Tafakari ya Sala ya Malaika wa Bwana, Jumapili tarehe 6 Aprili 2014 kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican anasema kwamba, ufufuko wa Lazaro lilikuwa ni tukio kuu kabisa lililofanywa na Yesu, ili kuwaimarisha wafuasi wake katika imani katika Fumbo la Mateso, kifo na ufufuko wake.

Baba Mtakatifu anasema hata leo hii Yesu bado anaendelea kuwalilia wale wanaoteseka katika kifo na dhambi, ili aweze kuwaonjesha huruma na upendo wake usiokuwa na kifani. Yesu anawaita waamini kutoka katika maisha ya dhambi, katika ubinafsi na anasa, ili waweze kuonja uhuru wa kweli pasi na kiburi. ufufuko wa mwamini unaanza pale anapoonesha utii kwa Yesu, ili kukimbilia mwanga na maisha mapya, kwa kutambua kwamba, wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.

Baba Mtakatifu anasema, huu ni mwaliko wa kutubu na kumwongokea Mwenyezi Mungu, kwani huruma yake haina mipaka. Yesu yuko tayari kutoa jiwe kwenye kaburi la maisha ya waamini; jambo linalowatenganisha na Kristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.