2014-04-05 15:50:59

Rais wa Liberia asifu mchango wa Jimbo la Papa


(Vatican Radio) Mapema Jumamosi , 5 March, Baba Mtakatifu Francisko, alitembelewa na Rais wa Liberia, Bibi Ellen Johnson Sirleaf. Baada ya kukutana na Papa , Rais Ellen pia alikutana na Katibu wa Vatican, Kardinali Pietro Parolin akiweko pia Askofu Mkuu Domeniquè Mamberti, Katibu kwa ajili ya Mahusiano na nchi za nje Vatican.

Salaam na majadiliano ya viongozi hao , vililenga zaidi uimarishaji wa mahusiano mazuri yaliyopo, kati ya Jimbo la Papa na nchi ya Liberia , pande zote mbili zikionyesha kuridhika na njia nzuri wanamotembea hasa katika mifumo ya kufanikisha demokrasia nchini Liberia.


Na kwa namna ya kipekee Rais Sirleaf, alisifu kazi za Kanisa katika ufanikishaji wa amani na maridhiano ya kitaifa na kwa mchango wake mkubwa katika ustawi wa jamii, elimu, demokrasia na maendeleo kwa ujumla. Na mwisho walizitazama kwa pamoja hali halisi za kimataifa na kwa namna ya kipekee katika mkoa wa Afrika Kaskazini Magharibi wakifanya rejea katika vipeo kadhaa vinavyoathiri eneo hilo.


Rais Ellen Johnson Sirleaf, wa Liberia ni mwanamke wa kwanza Afrika, kuwa Mkuu wa nchi, na Mshindi wa Tuzo ya Heshima ya Amani pia ni Mwenyekiti mwenza wa Jopo la ngazi ya juu la watu mashuhuri linalo jadili agenda za Maendeleo baada ya kutimia kwa Malengo ya milenia 2015 . Kwa sasa kuna andaliwa Malengo mengine yatakayo kuwa dira ya utendaji katika kipindi cha miaka kumi na mitano ijayo.


Rais Sirleaf, katika mkutano wake na waandishi wa habari, uliofanyika katika Makao Makuu ya Shirika la Chakula Duniani (WFP) siku ya Ijumaa, kwa lengo la kuzindua malengo ya ufanikishaji uhakika wa chakula na lishe katika kaya, agenda za baada mwaka 2015, alisema, maelezo ya Papa Francisko juu ya suala la umaskini ni makini na ya nguvu.

Na kwamba , maneno ya Baba Mtakatifu Francisko yataendelea kutoa mwangwi tena na tena, katika mifano mingi, na inatoa msukumo wa nguvu, katika kushughulikia suala la umaskini kama jambo muhimu kwenye agenda zote za maendeleo

Na kwamba, mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa WFP , IFAD na FAO alisisitiza, yanabaki kuwa vyombo vya lazima vya kimataifa katika suala la kulisha dunia kama ni suala la kimataifa kwa ajili ya uhakika wa chakula kufanikishwa. Akizungumzia suala hili la chakula katika nchi yake mwenyewe, Rais alisema kuna hatua zilizopigwa ingawa juhudi zaidi bado zinahitajika.


Liberia imeboresha uhakika wa chakula katika kiwango cha asilimia 43 kutoka asilimia 38. Rais anatambua kiwango hicho bado ni cha chini, na hivyo watu wengi bado wanakabiliwa na njaa hasa katika maeneo ya vijijini.


Rais Sirleaf pia ylionyesha haja ya kutoa kipaumbele baada ya kutimia muda wa Malengo ya millenia yanayoishia 2015 kwamba, ajenda ya maendeleo ni si tu kupunguza umaskini lakini hasa ni kuelnga katika kuutokomeza umaskini katika kila hali na aina ya mfumo wake. Na kumekuwa na makubaliano ya jumla kwamba, ingawa masuala ya Malengo ya Maendeleo ya Milenia yamekuwa na mafanikio katika baadhi ya vipengere, bado kunahitajika kufanyika maboresho katika maisha ya watu 840,000,000 waliobaki katika sugu njaa duniani.








All the contents on this site are copyrighted ©.