2014-04-04 14:41:40

Tafakari ya nne ya Padre Cantalamessa:imani katika Yesu Kristu, Mungu kweli na mtu kweli


Wiki la nne la Mahubiri ya Kwaresima kwa Papa na Padre Cantalamessa “Imani katika Yesu Kristo, Mungu kweli na mtu kweli”.

Padre Raniere Cantalamessa , Ijumaa hii alitoa mahubiri ya nne ya kwaresima kwa Papa na wafanyakazi wa ofisi za Curia ya Roma. Mahubiri hayo aliyagawa katika vipengere vinne:
Kwanza amekizungumzia kipengere kinacho unganisha Makanisa ya Magharibi na Mashariki, juu ya Yesu Kristo, akisema ni muhimu kutambua kwamba kuna njia kadhaa zinazoelekea katika hatima moja tu nayo ni Yesu Kristu. Baadhi wanapendelea kuchukua mbinu na njia za tangu mwanzo wa Ukristu, yaani kusoma Bibilia. Pia , njia hiyo imegawanyika, kwa mara kadhaa kumfikia Yesu, , kwa mfano. Kuna wale wanaoanza moja kwa moja kwa kusoma kitabu cha Biblia, na kumfuata Yesu kwa namna yao, ambamo namo unaweza kufuata njia mbalimbali kwa njia zilizotumiwa na wakongwe utoaji wa Katekesi juu ya yaliyoandikwa na kanisa , katika mwanga wa Neno na unabii wa Yesu tangu wakati wa Agano la kale , katika njia yake ya kihistoria yenye kuhuisha maendeleo kumwamini imani, kwa kutazama tamaduni mbalimbali za maisha ya mazingira yaliyoandikwa pia katika Agano Jipya. .

Padre Cantalamessa anasema , Aidha Wakristu wanaoanza kwa kutafakari maisha ya watu na mahangaiko na mateso yao , ya kila siku leo hii , akilinganisha na uzoefu wa maisha ya Yesu na Biblia, katika kumgundua hasa Yesu yuko wapi. Ni kwa kumtambua yeye aliyofanywa kuwa binadamu na kuja kukaa kati yetu ambaye amechukua juhudi za kutushindia dhambi zetu , huyu ndiye Kristu, Mungu kweli na binadamu kweli katika nafsi moja.

2. Padre Cantalamensa katika kipengere cha pili alizungumzia juu ya Yesu wa Kihistoria na Kristu aliyaunganishwa tena katika mafundisho sadikifu ya Kanisa, akisema kwamba, Ukweli halisi wa Yesu ulipita katika kipindi na majadiliano na ukosoaji mkali katika karne mbili za mwanzo wa Ukristu ambamo mlikuwa na lengo la kuondoa yale yaliyofikiriwa kuwa ni dhania tu za ugunduzi wa kiteolojia.

Lakini juu ya mada hii uliweza kukamilika ka kuthibitisha mwendelezo kati ya Yesu wa Kihistoria Na Yesu anayetangazwa daima, Bado tafiti zinazofanywa kuthibitisha mwendelezo kati ya Kristo wa kerygma na Mafundisho ya Kanisa.

Padre Cantalamessa amehoji iwapo, utaratibu wa Mtakatifu Leo Mkuu na Imani ya Kaldea, zinaweka alama ya maendeleo madhubuti ya imani kaiak Agano Jipya au iwapo badala yake , inawasilisha utengano

Pia amezungumzia ziada ya kuwa na kanuni akisema kwamba, kwa zaidi ya karne nne na nusu wanateolojia wamekuwa wakifanya kazi ya ziada kutoa katika kanisa kanuni kwamba Yesu Kristo alikuwa ni Mungu na Mtu mkweli. Au kwa kifupi alikuwa mtu mwenye kuwa na asili mbili. Na maandiko yenyewe yanatuambia kuhusu nafasi ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya ufahamu wa Yesu kweli.







All the contents on this site are copyrighted ©.