Papa ahimiza Maaskofu wa Rwanda kuwa vyombo vya maridhiano.
Vatican Radio) Papa Francisko mapema Alhamis hii alikutana na mazungumza na kikundi
cha Maaskofu wa Rwanda ambao wako katika hija ya kitume hapa vatican , “ad limina
visit” . Katika hotuba yake iliyoandaliwa kwa ajili ya tukio hili, Baba Mtakatifu
Francisko, alikumbua mauaji ya kimbari yaliyotokea 1994, miaka 20 iliyopita, akisema,
kwa moyo wake wote, anaungana na Maaskofu na Wanyarwanda wote, katika kumbukumbu
hii ya kusikitisha na kutisha. Na aliwahakikishia maombi na sala zake kwa ajili
yao wenyewe , kwa jamii yao na kwa waathirika wote na familia zao, na anyarwanda
wote , bila kujali dini , kabila siasa.
Baba Mtakatifu aliendelea kusema kwamba
, miongo miwili baada ya matukio hayo kutisha , maridhiano na uponyaji wa majeraha
y akiroho na ubinadamu, yanapaswa kubaki kipaumbele katika utume wote wa Kanisa,
nchini Rwanda.
Na Hivyo aliwahimiza Maaskofu kudumisha dhamira yao na uwajibikaji
katika juhudi za uponyaji na maridhiano ya kitaifa. Na kwamba, Msamaha wa dhambi na
maridhiano ya kweli ,ni zawadi ya Kristo ambayo inawezekana kupokewa na kila binadamu,
ata kama inaweza kuonekana kwa macho ya kibinadamu kama jambo lisilo wezekana kutokana
na mateso kama hayo waliyo yaishi watu wa Rwanda, katika kipindi hicho cha vurugu
na mauaji ya kimbari. Papa ameonyesha kutambua kwamba, safari hii ya maridhiano kamili
inaweza kuwa ndefu na yenye kuhitaji uvumilivu, mazungumzo na kuheshimiana. Papa
Francis alisema , Kanisa katika nafasi yake , hivyo , linawajibika kutembea pamoja
na watu hadi mwisho wa safari hii, kuwafariji na kuwapa matumaini bora kwenye njia
hii ya mapatano ya kitaifa, kwa nguvu zao zote na katika imani yao na katika tumaini
lote la Kikristo. Na aliiongeza kusonga mbele na hatua hii kwa kasi zaidi , hasa
kwa njia za utoaji wa ushuhuda wa kweli mara kwa mara.
Wito kwa Maaskofu
pia uliwataka Maaskofu kuonyesha mchango wa Kanisa kwa ajili ya manufaa ya wote,
na kwa makini hususani katika mlengo wa elimu kama ufunguo Mkuu wa hali ya nchi kwa
siku za baadaye. Papa Francis alisema, " Kwa hiyo ni wajibu wa Kanisa kuunda watoto
na watu vijana, walio iva katika maadili ya Injili, na kuchota uzoefu hasa kwa neno
la Mungu , ambalo ni dira inayoonyesha njia ya amani,mapatano na umoja..
Pia
Papa Francis pia alizungumzia umuhimu wa jukumu la walei katika uinjilishaji na
ujenzi wa mshikamano katika jamii , akisema kwamba, Maaskofu wanapaswa kutoa kipaumbele
kwa mafunzo na msaada kwa watu wa kawaida, kwenye vyote, maisha ya kiroho na katika
maisha ya kibinadamu na akili, na malezi bora.
Papa Francis alihitimisha kwa
kuomba Msaada wa Mama Yetu ,Bikira Maria wa Kibeho, awaangazie wote. Upendo wa Maria
kwa ajili ya watoto wake, hasa maskini zaidi na walio jeruhiwa kijamii, na kwa ajili
ya Kanisa la Rwanda - na zaidi - kumgeukia kwa ujasiri, Mama yetu wa Huzuni ,ili
kwa maombezi yake , Rwanda na dunia zima , ipate kupokea zawadi ya maridhiano na
amani .