Papa na washauri wake wachambua Waraka wa Injili ya Furaha
Baba Mtakatifu Francisko, Jumanne tarehe Mosi, Aprili 2014 amekutana na kuzungumza
na viongozi wakuu wa Mabaraza, Halmashauri na Taasisi za Kipapa mjini Vatican. Agenda
kubwa ya kikao hiki ilikuwa ni kufanya upembuzi yakinifu, tafakari na ushauri ulioibuliwa
kutoka katika Mabaraza hayo kuhusu Waraka wa Kichungaji wa Baba Mtakatifu Francisko
Evangelii Gaudium, Furaha ya Injili.
Katika mkutano huu, viongozi hawa wakuu
wameangalia jinsi ambavyo Mama Kanisa anaweza kuumwilisha ujumbe huu katika maisha
na utume wake. Mkutano huu ulianza hapo saa 3:30 asubuhi na kuhitimishwa saa 6:00
mchana kwa sala ya Malaika wa Bwana.