2014-04-01 09:47:26

Kenya yadhibiti wakimbizi kutoka Somalia


Wakimbizi kutoka Somalia wanaohifadhiwa nchini Kenya watalazimika kukaa kwenye kambi mbili maalum zilizotengwa kwa ajili ya wakimbizi. Hayo yamebanishwa hivi karibuni na Waziri wa mambo ya ndani wa Kenya Bwana Joseph Ole Lenku kama sehemu ya mchakato wa kudhibiti mashambulizi ya kigaidi yanayoendelea kutishia maisha na usalama wa wananchi wa Kenya.

Kikundi cha Kigaidi cha Al Shabaab chenye makao yake makuu nchini Somalia, kimekuwa kikiendesha mashambulizi ya kushutukiza nchini Kenya na hivyo kusababisha hofu na wasi wasi mkubwa nchini humo. Tangu sasa wakimbizi kutoka Somalia watalazimika kuishi kwenye Kambi Dadaab na Kakuma. Kuna zaidi ya wakimbizi laki nne wanaoishi kwenye Kambi la Daab na wengine 125, 000 wanaishi kwenye Kambi ya Kakuma.







All the contents on this site are copyrighted ©.