2014-04-01 09:34:21

Hali ni tete Sudan ya Kusini!


Zaidi ya wananchi millioni moja kutoka Sudan ya Kusini, wanaoishi kwenye kambi za wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi maalum, wako hatarini kupoteza maisha yao kutokana na baa la njaa na magonjwa ya mlipuko, ikiwa kama hali ya sasa haitafanyiwa maboresho makubwa.

Sudan ya Kusini ambayo inakabiliwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe inaweza kujikuta katika hali tete zaidi kutokana na mvua zinazoanza kunyeesha nchini humo. Watoto, wanawake na wazee ndio watakaoathirika na hali hii ikiwa kama hakuna hatua makini zitakazochukuliwa na Jumuiya ya Kimataifa.

Hayo yamebanishwa na Bwana Yasmin Haque, mkurugenzi msaidizi wa Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa, UNICEF, baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi nchini Sudan ya Kusini, hivi karibuni.







All the contents on this site are copyrighted ©.