2014-03-31 16:32:11

Papa atahadhalisha: msiwe watalii katika safari ya imani


Papa Francisko , mapema Jumatatu hii, akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta alionya Mkristu kuwa na tabia ya kutangatanga kimaisha hasa maisha ya kiroho. Alitoa wito kwa Wakristo wote kulenga moja kwa moja, katika kuzifuata ahadi za Mungu, na kamwe kutokata tamaa.

Katika homilia hii amesema , kuna Wakristo aminifu kwa ahadi za Mungu, katika maisha yao ya kila siku. Na pia kuna wale wengine ambao imani yao kimaisha huyumbayumba, na bado kuna wengine wanao songa mbele kwa kuifanya imani kama jambo la mpito.

Papa Francesco, ameelezea tofauti zilizopo kati aina hizi tatu za waumini , akisema inasaidia kuelewa kwamba, maisha ya Kikristo ni safari au hija ya kiroho. Papa alielezea kwa kurejea somo la kwanza, lililosomwa kutoka Kitabu cha Isaya, akifafanua kwamba Mungu daima, hutimiza ahadi zake, kabla ya mengine yote. Na ahadi yake ni uwepo wa maisha mapya, tena maisha yenye furaha kamili ." Na kwamba, msingi mkuu katika hili ni fadhila ya matumaini , na imani katika ahadi ya Mungu . Hiki ni kiini cha maisha ya kikristo. Papa amewataka waamini wasikate tamaa kutembea katika njia hii ya imani licha ya magumu na changamoto wanazoweza kupambana nazo.

Kwa bahati mbaya, aliendelea kueleza , kuna wale wanaingia Ukristu, na baadaye huchoka na kujitoa. Wakristo hawa ni wengi! Wanakosa matumaini na kukata tamaa. Wao wanaamini, kutakuwa na Mbinguni na yote yatakuwa mazuri . Lakini wanashindwa kuifuta kwa uaminifu, njia inayoelekea katika ahadi hii. Wao hukamilisha amri, maagizo na kila kitu , lakini wamesimama kando, na hivyo Bwana hawezi kuwafanya kuwa chachu, kwa sababu wao hawatembei pamoja na Wakristo wengine . Na hili ni tatizo. Na kuna wengine kati yao, ambao hukosea njia ,kama ilivyo kwetu sote, na kutenda dhambi. kwa hawa tatizo hasa ni kule kutorudi katika njia, baada ya kutambua kuwa wako nje ya njia, yaani kutotubu na kumrudia Bwana.

Papa alieleza akilenga katiak somo la Injili, mbamo mtu mwenye imani anamwomba Yesu amponye mtoto mgonjwa. Mtu huyo, alisadiki laichoambiwa na Bwana na kujiunga katika mwendo wa kuelekea nyumba kwake bila wasiwasi wala mashaka na muda. alisubiri kwa imani kwamba manae atapona. Papa amewaasa kwamba, Bwana anatuomba kama waamini sote tuungane pamoja na kutembea katika njia moja ya kuuelekea Ufalme wake, Tusiipoteze njia kwa kufuata njia zenye furaha za mpito katika maisha. Bwana anatutaka leo hii, tuyageuze maisha yetu na kuzitazama ahadi za Bwana , kuwa watu wa Imani katika ahadi za Mungu.

Na kwamba Kwaresima ni wakati mzuri wa kufikiria kama tuko katika njia au nje ya njia. Leo hii ni wakati wa kukata shauri na kujiunga katika barabara hii, kusonga mbele na mwendo wa imani kwa ushupavu zaidi na zaidi, na si kuwa na teolojia ya utalii, ya kuzunguka huko na kule, bila ya kusonga mbele kiimani.










All the contents on this site are copyrighted ©.