2014-03-31 11:30:19

Monsinyo Brian Ferme ateuliwa kuwa Katibu wa Sekretarieti ya Uchumi mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Brian Ferme kuwa Katibu wa Sekretarieti ya uchumi iliyoanzishwa hivi karibuni mjini Vatican na Mwenyekiti wake ni Kardinali George Pell na Mratibu mkuu ni Kardinali Reinhard Marx. Kazi kubwa itakayofanywa na Monsinyo Brian Ferme ni kumsaidia Mratibu kutekeleza majukumu yake ya Baraza la Kipapa la Uchumi ambalo limepewa dhamana ya kuratibu na kushughulikia masuala yote yanayohusu utawala, fedha na uchumi mjini Vatican.

Monsinyo Ferme alizaliwa kunako mwaka 1955 ni Padre wa Jimbo Katoliki la Portsmouth,Uingereza. Alisoma falsafa, taalimungu na sheria za Kanisa huko Melbourne, Oxford na Roma. Ni mwandishi maarufu wa vitabu na mala kwenye majarida ya kimataifa. Amekuwa jaalimu wa Sheria za Kanisa Chuo Kikuu cha Kipapa cha Gregorian na Laterano. Amekuwa ni “Dean of Studies” Kitivo cha Sheria za Kanisa Chuo Kikuu cha Kikatoliki Marekani kunako mwaka 2003 na baadaye, alihamia Venezia kuwa ni mkuu wa Kitivo cha Sheria za Kanisa cha Mtakatifu Pio wa kumi.

Kwa miaka mingi Monsinyo Ferme amekuwa ni mjumbe wa Mabaraza kadhaa ya Kipapa mjini Vatican hasa zaidi kama mshauri wa Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa pamoja na Baraza la Kipapa la Sheria za Kanisa.








All the contents on this site are copyrighted ©.