2014-03-29 11:40:42

Kardinali Pietro Parolin, kuchangia utafutaji wa suluhu ya amani nchini Venezuela


Wananchi wa Venezuela wanaendelea kukabiliana na hali tete katika kipindi hiki cha historia ya maisha ya nchi yao. Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican anasema, Vatican inaendelea kufuatlia hali ya machafuko ya kisiasa nchini Venezuela na kwamba, kuna uwezekano mkubwa kwa Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kutoa mchango wake katika mchakato wa kutafuta suluhu ya machafuko ya kisiasa nchini Venezuela yanayoendelea kusababisha maafa makubwa kwa watu na mali zao.

Kardinali Parolin anaifahamu vyema Venezuela na anawapenda wananchi wake, anaendelea kufanya upembuzi yakinifu, ili kuangalia jinsi gani Kanisa linaweza kuchangia katika upatikanaji wa suluhu ya mgogoro wa machafuko ya kisiasa nchini Venezuela.







All the contents on this site are copyrighted ©.