Idhaa ya Kiswahili ya Redio Vatican inapenda kuwatangazia wasikilizaji wa Afrika Mashariki
na Kati kwamba, tangu Jumapili 30 Machi 2014, kipindi kitasikika katika masafa tofauti
na ilivyo sasa. Kipindi kitasikika katika masafa ya kHz 13765(21.799mb) au khz 15370
(19.51mb) muda ni uleule saa moja za jioni. Kipindi hicho kitasikika tena kesho
yake katika ya Masafa mafupi ya Khz, 7360( mbd 40.76 )au kHz 9660 mb31.05 au kwa
njia ya satelite, majira ya kumi na mbili na nusu za asubuhi (saa za Afrika Mashariki).
Kwa wasikizaji wetu wa Roma, tangu Jumapili kipindi kitasikika katika masafa
ya FM 103.8, saa kumi na mbili kamili za jioni, na kitarudiwa kesho yake saa tatu
na nusu za asubuhi katika masafa hayo hayo FM 103.8 Ukisoma tangazo hili, tafadhali
mnong'onezee jirani yako. Tunaomba radhi kwa mabadiliko haya na kuwatakia usikilizaji
mwema.