Marehemu Waziri mkuu mstaafu Adolfo Suarez Gonzales atakumbukwa na wengi!
Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambirambi kwa Askofu Jesus Garcia Burillo
wa Jimbo Katoliki A'vila, Hispania kutokana na kifo cha Waziri mkuu mstaafu Adolfo
Suarez Gonzales mwenye umri wa miaka themanini na moja, aliyefariki dunia hapo tarehe
23 Machi 2014 na kuzikwa tarehe 24 Machi baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Katika
ujumbe ulioandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, katibu mkuu wa Vatican,
anaiombea roho ya Marehemu Waziri mkuu mstaafu Suarez, pumziko la milele. Huyu ni
kati ya viongozi mashuhuri nchini Hispania katika miaka ya hivi karibuni. Baba Mtakatifu
anapenda kutoa salam zake za rambi rambi kwa wote walioguswa na msiba huu pamoja na
kuwapatia baraka zake za kitume, akiwa na tumaini katika ufufuko wa wafu na uzima
wa milele.