Monsinyo Marek Zalewski ateuliwa kuwa Balozi Mpya wa Vatican nchini Zimbabwe na kupandishwa
hadhi kuwa Askofu mkuu
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Monsinyo Marek Zalewski kuwa Balozi mpya wa Vatican
nchini Zimbabwe sanjari na kumpandisha hadhi ya kuwa Askofu mkuu. Askofu mkuu mteule
Marek Zalewski alizaliwa tarehe 2 Februari 1963 huko Augustow, Poland.
Baada
ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 27 Mei 1989. Ana
shahada ya uzamivu katika Sheria za Kanisa. Alianza kutoa huduma za kidiplomasia mjini
Vatican kunako tarehe 1 Julai 1995 na kupangia huko: Jamhuri ya Afrika ya kati, Umoja
wa Mataifa, Uingereza, Ujerumani, Thailand, Singapore na Malaysia.