Hospitali ya Rufaa ya Nelson Mandela kwa ajili ya magonjwa ya watoto kuanza kazi 2017
Bara la Afrika linaendelea kumuenzi Mzee Nelson Mandela, aliyesimama kidete kulinda
na kutetea: haki na amani; ukweli na uwazi; demokrasia na mafao ya wengi ndani na
nje ya Bara la Afrika. Hivi karibuni, kumewekwa jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi
wa Hospitali ya Watoto, inayotarajiwa kuanza kufanya kazi ifikapo mwaka 2017. Hii
inatarajiwa kuwa ni Hospitali kubwa ya rufaa kwa ajili ya magonjwa ya watoto kutoka
katika nchi zilizoko Kusini mwa Afrika, itajengvwa mjini Johannesburg, Afrika ya
Kusini.
Itakumbukwa kwamba, Barani Afrika kuna Hospitali kubwa za rufaa kwa
watoto wagonjwa, huko Nairobi, Kenya na Cairo, Misri. Mchakato wa kuanzisha Hospitali
ya rufaa kwa ajili ya magonjwa ya watoto anasema Sibongile Mkabile, mkurugenzi wa
Hospitali hii ni kutaka kuokoa maisha ya watoto wadogo wanaoendelea kupoteza maisha
yao kutokana na ukosefu wa huduma makini. Hospitali ya Kumbu kumbu ya Nelson Mandela,
itakapokamilika itakuwa na vitanda 220.
Hii ni Hospitali ya binafsi, lakini
inayolenga kutoa huduma hata kwa familia maskini, kwani kwa kawaida huduma za matibabu
Afrika ya Kusini ni za ghali na mara nyingi wanaofaidika ni familia zenye uwezo mkubwa
zaidi wa kiuchumi.