2014-03-21 15:14:27

Padre Cantalamessa : Tafakari ya Pili kwa Papa na Wasaidizi wake wa karibu katika Idara za Curia.


(Vatican Radio) Baba Mtakatifu Francisko na wasaidizi wake katika ofisi za Curia ya Roma, mapema ijumaa hii, walikuwa na kipindi cha ukimya cha kusikiliza tafakari ya neno la Mungu kutoka kwa Padre Raniero Cantalamessa, Mhubiri katika Makazi ya Kipapa kwa wakati wa Kwaresima. Ijumaa hii ametoa tafakari yake ya pili kwenye mfululizo wa tafakari za Siku za Ijumaa, katika kipindi cha Kwaresima.

Tafakari ya Padre Cantalamessa , ililenga zaidi kwa Mtakatifu Agustino, chini ya Mada " Nasadiki Kanisa ni Moja Takatifu. Hotuba yake aliigawa chini ya vipengere vinne,1. Kuhama kutoka kanisa la Mashariki hadi Magharibi, 2. Kanisa ni nini 3. Ufunuo wa kikanisa wa Mtakatifu Agustine leo hii una maana gani . 4 Msharika wa Mwili wa Kristo, aliyehasishwa kwa Roho mtakatifu.

Katika maelezo yake, Padre Cantalamessa alirejea utangulizi wa tafakari ya wiki iliyopita ambamo walitafakari maana ya kipindi hiki cha kwaresima kwamba, ni wakati wa kwenda jangwani na Yesu, kufunga na vyakula na maonyesho ya picha zinazo onyeshwa katika runinga na vyombo vingine vya habari , na hivyo kujifunza kushinda majaribu, na juu ya yote, kukua katika kujenga uhusiano wa karibu na Mungu.

Na ameeleza kwamba katika mahubiri manne yaliyo salia, ataendelea kutafakari juu ya mada aliyoianza katika Kwaresima ya 2012 juu ya Mababa wa walimu wa Kanisa , na baada ya Mababa wa Kanisa la Kigriki kwa sasa anatazama kwa makini maelekezo yaliyotolewa na Mababa wa Kanisa waliofuatia , Mtakatifu Augustine, Mt. Ambrose , Mt. Leo Mkuu, Mt. Gregory Mkuu, kwa ajili ya kuona , nini kila mmoja wao anasema kwetu leo hii, kuhusu ukweli wa imani. Na kwa mtiririko huo, asili ya kanisa , uwepo halisi wa Kristo katika Ekaristi, Mafundisho ya Kanisa ya Kaldonia, na ufahamu wa kiroho wa maandiko.

Padre Cantalamessa anataja lengo la utajiri uliomo katika mafundisho ya walimu hawa wakuu wa kanisa, kuwa ni kuthibitisha uzuri na furaha ya kuamini , kama anavyosema Mtakatifu Paulo, kwa maana haki ya Mungu itadhihirisha ndani yake toka imani hata imani " (Rom 1:17), toka imani hata akili na moyo, na Mwenye Haki ataishi kwa imani. Inakuwa ni kuongeza kiwango cha imani ndani ya kanisa na hivyo kuwa chemichemi ya kutangaza neno la Mungu limwenguni kote.

Padre Cantalemessa aliendelea kuzungumzia mafundisho mbalimbali ya Mababa wa Kanisa , tangu nyakati za mwanzo wa kanisa katika mitazamo mbalimbali ya Utakatifu wa Kristo ,Roho Mtakatifu na Utatu Mtakatifu , na katika kumjua Mungu , kwamba mtu anaweza kuwa na hisia kwamba kulikuwa na mambo machache sana yaliyo bakia kwa Mababa wa Kanisa kufanya mabadiliko katika mafundisho sadikifu kwa Wakristo. Na kwamba, wakiwa wamehamasika kwamba wao ni sehemu ya utamaduni huo wa Kikristo, walikuwa na wajibu mkubwa katika kutoa maelekezo sahihi kwa Kanisa, wakichochewa na barua za Mtume Paulo , kutafakari juu ya mandhari ya neema , Kanisa , sakramenti, na maandiko Matakatifu .

Na akirejea ufunuo wa Mtakatifu Augustine kwa kanisa leo hii anasema , kuna mabadiliko makubwa duniani na katika kanisa na hata kiteolojia tangu wakati ule wa Mtakatifu Agustine. Na hivyo kwa Mkristo ni suala la kuanza kutazama upya na kwa unyenyekevu wa nyakati , kwa ajili ya kuugundua upya yalifumbatwa katika utu wa Kristo. Tunahitaji kujiweka katika wakati ule wa Mitume , waliopambana na ulimwengu wa kipagani, kama ilivyo kwa wakati huu Kanisa linakabiliana na watu wakristu walioasi.

Mtume Paulo kwa maneno mafupi alisema, kazi ya thamani ya Mkristo ni kuitangaza Injili ya Kristu aliyesulubiwa na kufufuka. Na hii haina maana kwamba ni kupunguza ukuu wa teolojia na utajiri wa kiroho unaotokana na marekebisho yanayofanyika au kurudi katika taratibu na kanuni za awali , bali kama njia ya kuruhusu Ukristu kuwaleta watu wengi zaidi ndani ya kanisa ambalo ni Mwili wa Kristo mwenyewe.







All the contents on this site are copyrighted ©.