2014-03-20 15:17:12

Kardinali Tomko adhimisha miaka 90 ya kuzaliwa.


Jumanne jioni, katika Kanisa dogo la Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbanian, Roma, Kardinali Fernando Filoni, Mkuu wa Decania ya Makardinali, aliongoza Ibada ya Misa, kwa nia ya kumtolea Mungu shukurani, kwa Kardinali Josef Tomko , kutimiza miaka 90 ya kuzaliwa. Katika kanisa hilo Kardinali Tomko amefanya Ibada ya aina hii ya kusherehekea Siku Kuu ya Kuzaliwa kwa mara 16.

Shirika la habari la Fides , limetaarifu kwamba, Kardinali Josef Tomko aliisherehekea miaka yake 90 ya kuzaliwa, akiwa amezungukwa na mrithi wake katika huduma ya Umisionari, Kardinali Fernando Filoni, na Makardinali wengine akiwemo Kardinali Angelo Sodano, Maaskofu wakuu na Maaskofu, Mapadre , Watawa na marafiki zake wenye wanaoendelea kuwa nae karibu katika utumishi wake kwa muda mrefu kwa Kanisa. Aidha, walikuwepo wafanyakazi wa Usharika kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu , Taasisi ya Kipapa kwa ajili ya Misioni, pamoja na wengine wengi.

Kardinali Filoni , katika homilia yake alitoa shukurani zake za dhati kwa Kardinali Tomko, kwa yale aliyoyafanya na yale ambayo bado anatarajia kuyafanya kwa ajili ya kujenga umoja kamili wa kanisa na kwa mchango wake hususani katika kazi za kimisionari .

Amesema, tunamshukuru kwa ajili ya mbegu nzuri aliyoipanda katika Kanisa, na kwa ushuhuda wake katika maisha ya kipadre, na hivyo wakati wa sherehe hii, kwao unakuwa ni wakati muafaka wa kutafakari nini maana ya maisha ya Kardinali Tomko katika kanisa na jamii kwa ujumla. Kardinali Tomko alizaliwa( Machi 11 1924) na alipadirishwa ( Machi 12, 1949 ), kufanywa Askofu ( Septemba 15, 1979 ). Hivyo ametimiza miaka 65 ya upadre na miaka 35 ya kuwa Askofu.
Kardinali Filoni, aliendelea kutoa wasifu mfupi wa Kardinali Tomko kwamba , katika miaka yake tisini ,akiwa mzaliwa wa tafa lake pendwa la Slovakia, kwamba katika miaka ya ’40, alikamilisha masomo yake katika Chuo Kikuu cha Gregorian na Lateran ambako alijipatia shahada katika Teologia, sheria za kanisa, na Sayansi ya jamii. Wakati huo taifa lake lilikuwa katika giza nene la Ukomunisti na Slovakia ikiwa chini ya himaya Urusi. Na kwa miaka miaka 15 yalikuwa ni makamu wa gombera wa Chuo cha Kipapa Nepomuceno , kabla ya kuwa Chini ya Usharika kwa ajili ya Maaskofu , na kisha, tangu mwaka 1979 , alifanywa kuwa Katibu Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu. Na alitajwa kuwa Askofu na Mwenyeheri Yohana Paulo II tarehe 15 Septemba 1979. Baada ya miaka 6 , Aprili 24, 1985 aliteuliwa na Papa kuwa Mkuu wa Usharika kwa Uinjilishaji wa Watu , na wakati huo huo, Kansela wa Chuo Kikuu cha Kipapa Urbaniana. Katika mwaka huo huo , Mei 25, 1985, akawa Kardinali Shemasi.

Kadi. Filoni alieleza katika miaka yake 16 ya kuliongoza Shirika kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu, aliweza kufunga safari nyingi katika utume wa kimisionari, na alitoa msukumo mkubwa kwa maisha ya utume wa kimisionari hasa uimarishaji wa Makanisa vijana na majimbo mengi ya Afrika, Asia, Oceania na Amerika.









All the contents on this site are copyrighted ©.