2014-03-20 13:52:14

Jifunzeni kushukuru!


Shukrani huainisha sala ya Kanisa ambalo kwa kuadhimisha Ekaristi Takatifu hujifunua lilivyo na huwa kamilifu zaidi. Kwa kweli, katika kazi ya wokovu, Kristo huvifanya viumbe huru kutoka katika dhambi na mauti ili kuvitakasa upya na kuvifanya vimrudie Mungu Baba kwa ajili ya utukufu wake. Shukrani ya viungo vya Mwili hushiriki shukrani za Kichwa chao.

Mtakatifu Paulo anawahimiza Wakristo kushukuru kwa kila jambo kwani hayo ni mapenzi ya Mungu kwao kwa njia ya Yesu Kristo. Anawataka waamini kudumu sana katika kuomba, wakikesha katika kuomba huku wakishukuru.

Baba Mtakatifu Francisko wakati huu anapohitimisha Mwaka mmoja tangu alipochaguliwa kuliongoza Kanisa Katoliki, anawaalika watumiaji wa mitandao ya kijamii kujifunza kumshukuru Mungu pamoja na jirani. Hii ni dhana ambayo wazazi na walezi wanapenda kuwafundisha watoto wadogo, lakini watu wazima wenyewe wanasahau kushukuru!







All the contents on this site are copyrighted ©.