Kati ya mambo yanayoendelea kupewa kipaumbele cha pekee na Baba Mtakatifu Francisko
ni upendo kwa Mungu na jirani; umuhimu wa kuchuchumilia huruma ya Mungu kama njia
ya kujitakasa na kuyatakatifuza malimwengu. Maskini na wote wanaosukumizwa pembezoni
mwa Jamii kutokana na umaskini wa: hali na kipato; maadili na maisha ya kiroho, waonjeshwe
upendo wa Mungu usiokuwa na mipaka kwa waja wake.
Baba Mtakatifu Francisko
katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema kwamba, upendo wa
Kikristo hauna mipaka. Haya ndiyo mafundisho yanayotolewa na Yesu Kristo, kielelezo
cha Msamaria mwema.