2014-03-19 12:51:24

Tamko la Maaskofu lasema: Papa Francisko hatatembelea Uganda mwaka huu.


Askofu Mkuu John Baptist Odama wa Jimbo Kuu la Gulu na Mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Katoliki Uganda,kwa niaba ya Baraza la Maaskofu Katoliki Uganda , anawafahamisha Wakristu wote wa Uganda na dunia kwa ujumla kwamba, Papa Francisko, pamoja na kupokea kwa moyo mkunjufu mwaliko wa kuitembelea Uganda wakati wa maadhimisho ya Jubilee ya miaka hamisini tangu wafia dini wa Uganda kutangazwa kuwa Watakatifu,kutokana na msongamano wa shughuli zingine zilizokuwa zimeandaliwa awali, kwa mwaka huu hataweza kwenda Uganda kuongoza sherehe za Jubilee hiyo, iliyokuwa imepangwa kufanyika tarehe 18 Oktoba 2014. .

Taarifa inabaini, Septemba 2013, Maaskofu Katoliki wa Uganda walituma mwaliko wao kwa Papa Francisko wakimwoba aitembelea Uganda, kuhitimisha Maadhmisho ya Jubilee ya kutimia miaka 50 tangu wafia dini wa Uganda kutangazwa Watakatifu.

Baada ya kupata jibu la mwaliko wao, Maaskofu ya tarehe 14 March 2014,waliandika barua kuwafahamisha waamini kwamba, Papa Francisko hataweza kwenda Uganda mwaka huu, kutokana na ratiba yake kuwa nzito. Na hivyo wameamua kuahirisha maadhimisho ya sherehe hizo kitaifa hadi hapo maelekezo mengine yatakapotolewa. Na hivyo kwa matumaini wanasali ili ratiba ya Papa, ipate hata mwanya mdogo wa kumruhusu kuitembelea Uganda, katika siku za hivi karibuni.

Pia Maaskofu katika barua yao, wametangaza kwamba, Siku Kuu ya Wafia Dini wa Uganda ambayo huadhimishwa tarehe 3 June itafanyika kama kawaida chini ya usimamizi wa Jimbo la Kotido.

Maaskofu wanawatakia waamini wote, utajri wa kiroho katika kipindi hiki cha kwaresima na baraka nyingi za Mungu.







All the contents on this site are copyrighted ©.