Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda ameagiza wananchi wa mji wa Kibaigwa, Mkoani
Dodoma kutunza vyanzo vya maji vinavyopatikana katika Wilaya ya Kongwa ili kuendelea
kupata huduma ya maji safi na salama ambayo ni huduma muhimu kwa mahitaji ya wananchi
wa Wilaya hiyo.
Amesema hayo Jumatatu, Machi 17, 2014, wakati akizindua rasmi
Mradi wa Maji uliojengwa na Kampuni ya China Hunan uliochimba Visima viwili vya maji
Safi na Salama vyenye urefu wa mita 101 katika Mji Mdogo wa Kibaigwa ikiwa ni sehemu
ya maadhimisho ya wiki ya Maji ambayo hufanyika kila mwaka, na mwaka huu maadhimisho
hayo kitaifa yanafanyika mkoani Dodoma.
Akizungumza na wananchi waliohudhuria
uzinduzi huo, Waziri Mkuu aliwaeleza kuwa chanzo hicho cha maji ni muhimu na ni utajiri
wa mji wa Kibaigwa ambao wananchi wa mji huo wameombwa kutunza vyema chanzo hicho
kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku.
‘‘Ni meelezwa kuwa visima hivi vinauwezo
wa kutoa maji lita 62 kwa saa“, Ni lazima mtafute njia ya kuwaeleimisha wananchi ili
muweza kuhifadhi upatikanaji wa maji safi na salama katika mji wa Kibaigwa kwa kuangalia
namna ya kujenga mazingira bora ya kutunza chanzo kile, alisema Waziri Mkuu.
‘‘Mradi huu ulianza kujengwa mwezi Machi 2011 na umekamilika mwezi Septemba, 2013
kabla ya mradi kuanza Mji mdogo wa Kibaigwa ulikuwa na wakazi wapatao 18,550 kati
ya hao Wakazi 8,904 tu, sawa na asilimia 48 ndio walipata huduma ya maji, kwa mradi
huu wa sasa asilimia 90 ya wananchi wa Kibaigwa wana uhakika wa kupata maji safi na
salama na zaidi ya wananchi elfu 13,000 wanauwezo wa kupata huduma ya maji hayo“,
alisema Waziri Mkuu.
‘‘Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama
katika Wilaya ya Kongwa ni asilimia 68 ukiondoa mji mdogo wa Kibaigwa na sasa kuna
miradi kumi katika vijiji kumi ambavyo ni Mkoka, Chigwengweli, Songambele, Malanje,
Igangwa, Mseta, Mlali Iyengu, Mlali Bondeni, Ngumbi na Pembamoto, miradi hii ikikamilika
itaongeza idadi ya watu wanaopata huduma ya maji Safi na Salama na kufikia asilimia
75 katika Wilaya ya Kongwa“, alisisitiza Waziri Mkuu.
Waziri Mkuu alisema,
Miradi hii ni kiashiria kuwa Serikali kupitia Ilani yake ya Chama Cha Mapinduzi inatambua
umuhimu wa sekta ya Maji kwa maendeleo ya Kiuchumi, Kijamii na hifadhi za mazingira,
hivyo Serikali itahakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kufikia asilimia 75
Vijijini na asilimia 95 Mijini ifikapo 2015.
Waziri Mkuu alisema, ‘‘nimesikia
kuwa ndoo ya lita 20 ni sh 20, ndoo ya lita 10 ni sh 10 na pipa ni sh 250“: Kwa utaratibu
huo ni vema uongozi wa Mji wa Kibaigwa kuangalia utaratibu wa kutunza fedha hizo kwani
kutakuwa na matengezo na marekebisho ya mashine pale zitakapo haribika, pia aliwaomba
kuanzisha utaratibu wa kutoa taarifa walau kila baada ya miezi mitatu ili wananchi
kupafamau mapato na matumizi ya huduma ya maji inayotolewa.
Vilevile, Waziri
Mkuu alisema Sera ya Maji ya mwaka 2002 inalenga katika kuhakikisha kuwa Wananchi
Vijijini wanapata huduma ya maji safi na salama kwa umbali usiozidi Mita 400 kutoka
kwenye makazi yao. Ii kufikia lengo hilo, Serikali kwa kushirikiana na Washirika
wa Maendeleo, Serikali za Mitaa, Wananchi na wadau wengine itaendelea kuboresha huduma
za maji vijijini kwa kujenga miradi mipya, kupanua na kukarabati miundombinu ya maji.
Maadhimisho ya Wiki ya Maji yalianza mwaka 1992 ambapo iliamuliwa kuwe na
kauli moja kuanzisha Wiki ya Maji Duniani. Mwaka huu Kimataifa yanafanyika Tokyo,
Nchini Japan.