Mheshimiwa Padre Antoine Sabi Bio ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Natitingou,
Benin
Baba Mtakatifu Francisko amemteua Mheshimiwa Padre Antoine Sabi Bio, aliyekuwa Msimamizi
wa Kitume Jimbo Katoliki la Natitingou kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Natitingou,
nchini Benin. Askofu mteule alizaliwa kunako mwaka 1963.
Baada ya masomo na
majiundo yake ya Kikasisi, akapadrishwa kunako tarehe 7 Desemba 1991 baada ya hapo
akaendelea na masomo ya juu Chuo Kikuu cha Wasalesiani wa Don Bosco, Roma na kuhitimu
masomo yake tarehe 19 Juni 2002. Tangu wakati huo amepangiwa majukumu mbali mbali
kama Msarifu wa Jimbo, Paroko, Gombera na Makamu Askofu.
Tangu Mwaka 2009
hadi mwaka 2013 Alikuwa Paroko. Mwaka 2011 aliteuliwa kuwa ni Msimamizi wa Kitume
Jimbo Katoliki Natitingou, Benin,, utume ambao ameuendeleza hadi kuteuliwa kwake kuwa
ni Askofu mpya wa Jimbo la Natitingou, Benin.